Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By | Blog Gadgets Via Blogger Widgets

Wednesday, May 8, 2013

Lwakatare, Ludovick wafutiwa mashitaka ya ugaidi




Mahakama Kuu ya Tanzania imefuta mashitaka yote ya ugaidi yaliyokuwa yanawakabili Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA Wilfed Lwakatare na mwenziye Ludovick Joseph.Taarifa zinasema Mahakama Kuu imebakiza shitaka moja tu, la kula njama ya kuteka na kudhuru, kosa  ambalo kimsingi ni la jinai na lenye dhamana.
Taarifa zaidi zinasema kuwa watuhumiwa wamerudishwa rumande kwa kuwa dhamana haikuwa imeandaliwa.
Katika kesi hii, Lwakatare anawakilishwa na jopo la mawakili watano ambao ni Mabere Marando, Tundu Lissu, Prof. Abdallah Safari, Peter Kibatala na Nyaronyo Kicheere.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...