Katibu
 Mkuu wa Zamani Ofisi ya Rais Ikulu,Mzee Timothy Apiyo (pichani), 
amefariki dunia katika hospitali ya Milpark nchini Afrika Kusini 
alikokuwa amelazwa.
Marehemu
 Mzee Apiyo alikuwa Katibu Mkuu wa Ikulu kwa Kipindi kirefu mpaka 
alipostaafu na kuhamia Kinyerezi jijini Dar es Salaam. Anatajwa kuwa ni 
mmoja wa viongozi waandamizi waliokuwa hawana masihara kazini, kiasi 
hata viongozi serikalini walikuwa wakimheshimu sana.
Mipango
 ya kuusafirisha mwili wa marehemu Mzee Apiyo inaendelea nasi 
tutawafahamisha kila hatua kwa kadri tutavyopata ripoti hizo.
Timothy
 Apiyo, alizaliwa katika wilaya ya Rorya, Tarafa ya Suba, mkoa wa Mara. 
Alipata elimu ya msingi na sekondari akiwa hapo na mwaka 1959 alijiunga 
na Chuo Kikuu cha East Afrika na kuchukua digrii ya kilimo.
Baada
 ya kuhitimu aliingia serikalini wakati huo Tanzania ikiitwa Tanganyika,
 na baadaye alijiunga na Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda. Mwaka 
1959 alihitumu Makerere na kupangiwa kufanya kazi katika Chuo cha Kilimo
 cha Ukiliguru.
Mwaka
 1960 alihamishiwa wilaya ya Muheza mkoa wa Tanga kuwa Bwana Shamba wa 
Wilaya na mwishoni mwa mwaka huo akahamishwa tena kwenda Wilaya ya 
Ifakara mkoani Morogoro ambako alikuwa Ofisa Mwandamizi katika Kituo cha
 Utafiti wa Kilimo cha Ilonga.
Alikaa
 Ilonga hadi Agosti 1962 ambapo alipata ufadhili wa kwenda kusoma 
Marekani katika Chuo Kikuu cha West Virginia ambako alichukuwa digrii ya
 pili ya Sayansi ya Kilimo na kutunukiwa cheti mwaka 1963.
Baada
 ya kurejea nchini, mwaka 1964 alipangiwa kufanya kazi Wizara ya Kilimo 
na baadaye akapelekwa Shinyanga kuwa Ofisa Kilimo wa Mkoa. Desemba 1965 
alihamishiwa mkoa wa West Lake (Sasa Bukoba). Na mwakan 1967 akarudishwa
 wizarani nikiwa Afisa Mipango Mwandamizi.
Mwaka
 1968 akateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Mipango Kilimo katika Wizara ya 
Kilimo na mwaka uliofuata 1969, akawa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya
 Nyumba, Ardhi na Maendeleo Mijini. Novemba 1969 alirudishwa tena Wizara
 ya Kilimo kuwa Katibu Mkuu na Aprili 1972 akapata uhamisho kwenda kuwa 
Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Viwanda.
Aprili 1974 Mwalimu Nyerere alimteua kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na Julai 1986 alistaafu kazi



No comments:
Post a Comment